Ticker

6/recent/ticker-posts

Adsterra ad

JINSI YA KUPIKA HALF CAKE NZURI

Half cake Mahitaji Unga wa ngano kikombe 1na1/2 (kama robo hivi) Sukari 1/4 kikombe Baking powder 1/2 kijiko cha chai Magadi soda (bicarbonate soda/baking soda) 1 kijiko cha chai Mafuta 2 vijiko vya chai Mafuta ya kukaangia Maji ya uvuguvugu kiasi Matayarisho Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa. dondoo muhimu:-👇👇👇👇👇 Jinsi ya kupika half keki zilizo pasuka na kuiva vizuri. 1.Hakikisha unatumia vipimo sahihi bila kusahau bicarbonate of soda(baking soda) hiki ndicho kiungo muhimu ktk half cake na baking powder...(hamira SI lazima kuweka kwa half cake za kula tu...labda ziwe za biashara) 2.Unga wako unapokanda uwe mgumu hata kidole kishindwe kupenya kwenye unga Hauhitaji kuikanda sana kama maandazi ukishashikana tu inatosha. 3.Weka half keki zako kwenye mafuta kabla hayajapata moto. 4.Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja.(unaeza kuepua ili yapoe chini...au ukaongeza mafuta ya baridi jikoni ) Chef nancy

Chapisha Maoni

0 Maoni

Ad Code

Responsive Advertisement