Ticker

6/recent/ticker-posts

Adsterra ad

MWALIMU ABAKA WANAFUNZI WATANO

Mwalimu wa kiume aliyejulikana kwa jina moja la Ngoitanile anayekaribia kuwa na umri wa miaka 60 anayefundisha Shule ya Msingi Mwembetogwa iliyopo Mtila Kata ya Matola Halmashauri ya Mji wa Njombe, amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za ukatili wa kuwaingiza vidole sehemu za siri Watoto watano wanaosoma darasa la kwanza na la tatu na kuharibu usichana wao. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Butusyo Mwambelo amethibitisha kukamatwa kwa Mtuhumiwa mara baada ya kupata taarifa za uficho na kwenda kumkamata. "Bahati nzuri tulikuwa na majina ya wale Watoto ambao wako watano, wawili ni darasa la kwanza na watatu ni wa darasa la tatu kwa hiyo tukafanya utaratibu wa kuwapeleka Hospitali na Daktari akatoa taarifa kwamba hao Watoto inaonekana sehemu zao za siri wameingiliwa na kitu butu hawana bikra” Amesema mara baada ya taarifa hizo walilazimika kuwahoji Watoto hao juu ya vitendo walivyofanyiwa ambapo waliweka wazi kuwa wamekuwa wakiingizwa vidole sehemu za siri na Mwalimu huyo wakiwa darasani huku wakati mwingine akiwaita ofisini “Kibaya zaidi walipoulizwa Wanafunzi wengine nao wamekiri kweli kwamba huyu Babu anafanya hicho kitendo mbele ya Wanafunzi wengine na lile darasa kuna Watoto wa kiume na wa kike, kwahiyo huyu Mwalimu yupo hapa Kituo cha Polisi lakini ushirikiano kwa walimu tumekosa wamesema hizo taarifa hawana ila watoto ndio wamesema" Kamanda Butusyo ametoa wito kwa Wananchi wa Njombe kuacha kuficha taarifa za matukio kama hayo na kutoa ushirikiano kwa Polisi huku akisema upelelezi unaendelea dhidi ya Mtuhumiwa na hakuna dhamana itakayotolewa kwake kwa sasa mpaka Mahakamani lakini sio Kituo cha Polisi. #MillardAyoUPDATES

Chapisha Maoni

0 Maoni

Ad Code

Responsive Advertisement