Ticker

6/recent/ticker-posts

Adsterra ad

JINSI YA KUPIKA UROJO MTAMU

JINSI YA KUPIKA UROJO MAHITAJI YA UROJO: ili kuweza kupika urojo vizuri unatakiwa uwena vitu vifuatavyo: Badia za (dengu au za kunde),kachori, chipsi za muhogo, mayai, mishkaki ya nyama. NB: hivi vitu nilivyo viorodhesha unaweza ukaandaa kiasi unacho kutaka mwenyewe. MAELEKEZO -kama ni urojo wa embe basi zichemshe baada ya hapo zivuruge aidha kwa kijiko au kwa mkono (hakikisha kokwa ya embe isiingie wakati unazivuruga) -chemsha maji kiasi kulingana na mahitaji yako mwenyewe (hakikisha maji yanachemka vizuri ) -weka unga wa ngano kwenye maji huku yanaendelea kuchemka koroga korogavizuri (hakikisha unga hufanyi madonge ) -baada ya hapo weka zile embe ulizo vuruga vizuri kisha endelea kukoroga vizuri -hatua ya mwisho ni kuacha uchemke urojo wako baada ya kuchemka vizuri epua urojo wako kisha unaweza kuweka urojo kwenye kibakuli na kuweka yale mahitaji nilio orodhesha hapo juu. NB: unaweza kuweka chumvi saizi unayo unayotaka au unaweza kuweka saladi kisha baada ya hapo unaweza kunywa urojo wako

Chapisha Maoni

0 Maoni

Ad Code

Responsive Advertisement